Mars ina Maji yanayotembea: NASA imebaini
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/mars-ina-maji-yanayotembea-nasa-imebaini.html
Mwandishi:
Juma Shabani.
Katika
utafiti wa hivi karibuni umeoendeshwa na NASA umebaini uwepo wa maji yenye
chumvi yanayotembea katika sayari ya
MARS. Utafiti huu umeongeza uwezekano wa uhai kuwepo katika saya hiyo
inayotambulika kama sayari Nyekundu.
“Leo,
tunafanya mapinduzi ya uelewa wetujuu ya sayari” alisema Mkurugrnzi wa masuala
ya sayansi ya sayari wa NASA bwana Jim Green akiwa makao makuu ya Washington.
Kwenye mkutano na waandishi wa habari Jumatatu hii. “Mars sio kavu, sio jangwa
kama tulivyodhani hapo kabla – baada ya mambo kadhaa, vimiminika vya maji
vimebainika Mars” aliongeza bwana Jim.
Kwa miaka
kadhaa wanasayansi wamekuwa wakitambua kuwa, kwenye sayari ya
Mars kuna barafu
lakini taarifa za kuwepo na maji yanayotembea imechukuliwa kama taarifa ya
kupendeza na maendeleo mazuri kuelekea maisha kwenye sayari hiyo.
Mifereji ya
giza imeonekana kwenye picha za kiuchunguzi zinazobainisha kutembea kwa maji.
Picha hizi zimechukuliwa kipindi cha kipupwe japo vipindi vingene vya mwaka
maji haya huganda na kutoweka na mifereji hiyo.
Bi, Mary
Beth Wilhelm wa NASA kuhusu uvumbuzi huo amesema “Matokeo yetu inaonesha zaidi
jinsi panavyoweza kuwa na maisha katika Mars tofauti na ilivyodhaniwa kabla.”
Jim Green
aliongeza “Na sasa tuna nafasi kubwa ya kuwa katika wasaa mzuri wa kuchunguza
hilo. (la maisha kwenye Mars)
Kwa
uchunguzi huu ni wazi kwamba, katika miaka ijayo au hata karne ijayo. Kuna
uwezekano wa binaadam au viumbe hai kuishi katika sayari ya Mars. Kiuchunguzi
hii ni hatua kubwa sana nay a kutia moyo.
Chanzo: Fox
News
