CHENGE: HATUCHAGUI VIONGOZI WA KUBEBA ZEGE



Mbunge wa Bariadi Andrew Chenge (CCM) amewataka wananchi wa jimbo lake kuchagua viongozi wenye sifa za uongozi na si vinginevyo.

Mh. Chenge alitoa kauli hiyo alipowahutubia wananchi wa kata ya Bunamhala jimbo la Bariadi leo Jumanne katika mkutano aliouita wa lala salama kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu siku ya jumapili.


“Nataka mchague viongozi wenye upeo wa mambo, wazoefu na wenye hoja za ushawishi kama mimi, msichague viongozi kwa kuangalia nguvu na vifua vikubwa uongozi sio mashindano ya mbio za baiskeli wala kubeba zege”Alisema Chenge kauli iliyoacha minong’ono miongoni mwa wananchi.

Mbali na kauli hiyo Mbunge huyo anayewania muhula wa tatu kuliongoza jimbo la Bariadi aliwaomba wanachi waliohudhuria mkutano huo kuhakikisha wanampa kura za kutosha ili akamilishe mambo aliyabakiza katika ahadi zake huku akitoa ahadi nyingine za kuboresha huduma za afya, miundombinu na elimu.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walimwomba mbunge huyo kuhakikisha anawasaidia kuondokana na umaskini na kuwaletea maendeleo zaidi jambo ambalo Mh. Chenge alisema atalishughulikia kama watamchagua tena huku akiwataka wananchi kuwa na subira kwa baadhi ya mambo kwani mambo mazuri hayataki haraka.

(Mbunge wa Bariadi Andrew Chenge akiwa katika mkutano wa hadhara kata ya Bunamhala jimboni hapo)

Na, Aloyce Mchunga

Related

Tanzania 8124620106420410296

Post a Comment

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress