Bugando yaanza upasuaji wa vichwa kujaa Maji kwa watoto.



 DAKTARI bingwa wa kitengo cha mifupa  kutoka hospiali ya rufaa ya Bugando bwana Gerald Mayaya amesema zaidi ya watoto elfu 4000 huzaliwa wakiwa na tatizo la vichwa kujaa maji na migongo wazi  kati yao 1000 hupata matibabu na 3000 hukosa huduma na kupelekea kufariki dunia.


Akizungumza juzi  wakati wakiwafanyia upasuaji watoto 26 wenye matatizohayo jinsi  ya kuweza kujikinga na maradhi hayo,daktari bingwa wa kitengo cha mifupa Mayaya alisema matatizo hayo ya kujaa maji vichwa na migongo wazi yamekuwa nitatizo kubwa yanayopoteza nguvu kazi ya Taifa.
"Ili kukabiliana na tatizo linalo wakabili watoto,mama anatakiwa kipindi anajiandaa kubeba mimba anatakiwa kutumia vidonge ya forciasdi na vyakula vyenye kuleta madini hayo ambayo yanamjenga mtoto pindi anapo kuwa tumboni,"alisema Mayaya.
Aidha Mayaya aliitaka jamii kuwafichua watoto walio na maradhi hayo ili waweze kupatiwa matibabu mapema kwakuwa matatizo hayo yanatibika na kumfanya mtoto awe kama wengine endapo atafikishwa muda muafaka katika kituo cha afya.
Nae mama wa mtoto Faraja Tido aliyezaliwa na uvimbe mdogo lakini umeleta madhala makubwa na kumpelekea kufanyiwa upasuaji Atu Ngendelwa alisema wanaume wengi wamekuwa wakowakataa watoto na kuwatelekeza. 
“Mimi nilopo jifungua mtoto wangu alikuwa ana uvimbe mdogo nilipo mpigia simu mume wangu nikamweleza mtoto anamatatizo anatakiwa kupelekwa Muhimbili alisema yeye kwao hakuna mtu mwenye matatizo hayo hiyo simtambui huyo ni wako,lakini nimefika  Bugando nikakuta na wanawake wengine walio na watoto wenye matatizo haya wametelekezwa

NA MANSOUR JUMANNE ,MWANZA

Related

Tanzania 2068585232346282669

Post a Comment

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress