Konisaga : kurejesha fadhila za CCM,Asema bora Lawama kuliko fedheha.
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/konisaga-kurejesha-fadhila-za-ccmasema.html
NA MANSOUR JUMANNE,MWANZA
MKUU wa wilaya ya Nyamagana Baraka kunisaga
amemuahidi Mgombea Mwenza wa nafasi ya kiti cha uraisi Samia
Suluhu,kuwa yeye pamoja na wakuu wa wilaya wenzake wa mkoa wa Mwanza
watahakikisha wanarudisha fadhila kwa Chama cha mapinduzi
kutokana nyazifa walizopewa na Chama hicho.
Akizungumza katika viwanja vya shule ya
sekondari Nyabulogoya siku ya Ijumaa Kunisaga Alimshukuru Samia na
Chama Chake kwa Kupewa Ukuu wa wilaya na CCM na amesema hata wao lazime
warejeshe Fadhila kwa Chama hicho kwa Kuwaletea Ushindi kwa njia yoyte,ili nao
wakistaafu wapate posho zinazo wastahili.
“Nimepewa ukuu wa wilaya na Raisi Kikwete na hivyo
lazima hata tutakapostaafu sie Wakuu wa wilaya tupate posho zetu na heshima .
“Sitaki kuondoka na aibu wakati CCM ndo imetupa
kazi,kwanza mimi ni mjumbe kamati ya siasa ya wilaya lakini ndio mwenyekiti wa
ulinzi na Usalama wa wilaya,hivyo kuanzia sasa mpaka siku ya matokeo kutangazwa
matokeo watu wasiwe na hofu”Alisema kunisaga.
Mkuu huyo pia alisema viongozi wa Chadema, bado
wanalitaka jimbo la Nyamagana wamekuwa wakiwahimiza wananchi kuwa baada
ya kupiga kura wasiondoke kwenye maeneo ya kuhesabia kura jambo ambalo yeye
amesema atahakiksha analishughulikia ipasavyo kama utatokea uvunjifu wa Amani
“Mh mgombea Mwenza mi nakuambia safari hii
bora lawama kuliko fedheha,nimesikia viongozi wa Chadema wanawaambia wananchi
wakishamaliza kupiga kura wakae kuzilinda kura sawa,ila wajue tu me na wakuu
wenzagu wa wilaya tisa za mkoa wa Mwanza Tumejiandaa vya kutosha “Alisema
Kunisaga
Nae Katibu wa Mkoa wa Mwanza CCM, Mtaturu
alipanda jukwaani na kumpokea microphone uku nae akisisitiza kwa
kusema tayari serikali imeongea hivyo yeye hana la kuongezea hapo.
