IRAN NA MAREKANI KWAFUKUTA
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/iran-na-marekani-kwafukuta.html
Ni baada ya Waziri wa mambo
ya Nje Kusalimiana kwa kushikana mikono na Rais Obama.
AFP inataarifu kuwa, Nchini
Irani kumeibuka hasira dhidi ya waziri wa mambo ya nje Mohammad Javad Zarif
ambaye nje ya mkutano wa umoja wa mataifa uliokuwa unaendelea makao makuu ya
umoja wa mataifa UN alisalimiana na rais wa Marekani Bw. Barack Obama.
Hali hii imepingwa vikali na
wabunge kadhaa japowasiri amethibitisha kuwa kukutana huko kumetokea kwa bahati
mbaya na kwamba haikupangiliwa wao kukutana.
“ Kwa ruhusa ya nani
wamekutana na Obama?” Bahram Biranvad alihoji. “mara ya mwisho waliongea na
Obama kwenye simu, na mara hii! Kwa ruhusa ya nani? Alihoji bwana Biranvad
kuhusu rais Rouhan kuongea na simu na rais wa Marekani.
Zarif pia alikumbana na
tuhuma toka kwa msemaji wa mahakama bwana Gholamhossen Mohsen Ejeie kama
ilivyotolewa na FARS. Bila kumtaja Zarif, bw. Ejeie alizungumzia suala la
kusalimiana na Obama kwa kusema, “Baadhi ya wapelelezi wanalipwa kwa kazi hiyo,
ila kuna wengine inabidi tuwape kila kitu kwa kazi hiyo ya kutupeleleza.
Anaandaa mazingira ya adui”
Pamoja na makubalina ya July
14 juu ya Nyuklia ya Tehran kufikiwa na nche zenye uchumi mkubwa duniani.
Kiongozi mkuu wa kidini nchini Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema Washington
itabaki kuwa “adui namba moja wa Iran”
Inataarifiwa kuwa,
kusalimiana kwa kushikana mkono huku kwa Zarif na Obama inaweza kuwa mara ya
kwanza kunakotambulika kati ya Rais wa Marekani na kiongozi yeyote wa ngazi ya
juu wa Iran tangu nchi hizi walipokuwa na mahusiano mabaya ya kidiplomasia
tangu mapinduzi ta kiislam ya Iran ya mwaka 1979.
Chanzo AFP
