Kkosi cha Uingereza Hadharani -Watatu wapya waitwa -Watatu waachwa
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/kkosi-cha-uingereza-hadharani-watatu.html
Kikosi cha
team ya taifa ya mpira ya Englid maarufu kama Three Lions kimetajwa na kocha
mkuu Roy Hodgson siku ya leo ambapo majina mapya yametokea akiwa ni pamoja na
Delle Alli aliyeitwa katika kikosi hicho. Mchezaji huyu kinda wa Tottenham
mwenye umri wa miaka 19 ameitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi hiki. Mwingine
aliyeitwa ni Danny Ings mshambuliaji wa Liverpool.
Wachezaji
watatu wakiwemo maarufu wameachwa kutokana na matatizo mbalimbali ya kiafya
ikiwa ni pamoja na Daniel Sturridge anaeendelea kuachwa, wakati Luke Shaw naye
kaachwa kutokana na majeruhi aliyoyapata. Mwingine aliyachwa na Jack Grealish.
Three Lions
imeshafuzu na inamalizia michezo ya mwisho na Eastonia na Lithuania.
Kikosi cha
wachezaji 24 kimeitwa na kocha Roy ambacho ni:
- Makipa:
Butland,
Hart, Heaton
- Mabeki:
Bertrand,
Cahill, Clyne, Gibbs, Jagielka, Jones, Smalling na Stones
- Wachezeshaji:
Dele Alli,
Barkley, Carrick, Lallana, Milna, Oxlade-Chamberlain, Shelvey na Sterling
- Washambuliaji:
Ings, Kane,
Rooney, Vardy, Walcott
Hiki ndio
kikosi cha wachezi 24 kilichotajwa na kocha mkuu wa Uingereza Roy Hodgson.
Mwandishi juma shaabani
Kimataifa
