Ojadact :Sheria za Utangazaji Zimekanyagwa
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/blog-post_1.html
Chama cha
waandishi wa habari wa
kupiga vita matumizi
ya dawa za kulevya na uhalifu tanzania (ojadact) kinachukua nafasi
hii kuongea nanyi waandishi wa
habari juu ya sheria ya
maudhui ya utangazaji ( the broadcasting
services content).
Ndugu
waandishi wa habari tunaelewa kuwa,
mamlaka ya utangazaji
tanzania (tcra) ni chombo kilichoundwa
kisheria na kina wajibu wa
kusimamia sekta ya utangazaji
nchini kama jinsi sheria no
12 ya mwaka 2003 iliyounda
chombo hicho.
Kwa
masikitiko makubwa tunawaambia ndugu waandishi wa habari kuwa,
sheria ilitangazwa kwenye gazeti la serikali Juni 26, 2015
na kuanza kutumika, heria hii
imekuwa ni kitanzi kikubwa
kwa tasnia ya habari nchini
kwani inanyima uhuru
wa vyombo vya habari (M&F) na haki ya
kupata habari(RTI) wakati wa kuelekea kwenye
uchaguzi mkuu wa Oktoba 25
mwaka huu, kama zilivyo
sheria za makosa ya kimtandao
na takwimu za mwaka 2015
pamoja na miswada ya
sheria ya haki ya
kupata taarifa na ule wa huduma za vyombo vya
habari ambayo ilizuiliwa kujadiliwa bungeni mwezi Juni, 2015.
OJADACT tumeitazama sheria ya
maudhui ya utangazaji(Broadcasting services) na kuona mapungufu yafuatayo:-
·
Sheria hiyo
haijahusisha wadau wa habari,
kama miongozo ya utungaji wa
sheria ndogo au kubwa unavyotaka, jambo linalotia shaka
na kupelekea kuwa kati ya sheria kandamizi
zinazotungwa kwa lengo lakuminya
uhuru wa vyombo
vya habari na haki
ya kupata taarifa(Infringe media
freedom and right to information).
·
Sheria hiyo ina inageuza
wajibu wa misingi ya kitaaluma
kuwa matakwa ya
kisheria na hivyo kufuta
maana ya weledi katika tasnia ya
habari, mfano kusisistiza
kazi na wajibu wa mwandishi kutekelezwa
kisheria. Rejea sehemu ya
pili ya sheria kifungu cha
4(a,b,c,d,f, na na g).
·
Sheria hii
inaingilia weledi wa tasnia
ya habari kwa kutotambua baadhi
ya vigezo vilivyowekwa na wanataaluma kama chanzo
cha habari(News values), kwani haitambui chanzo cha mtu
katika kutengeneza
habari(Prominence). Rejea kifungu
cha 4(i) ambapo kifungu hicho kinakataza vyombo vya habari
kuripoti tukio/matukio ambayo
yanamhusisha mtu moja kwa moja bila
kujali kuwa yawezekana tukio
la mtu likatengeneza habari na kuwa
na maslahi kwa umma.
·
Sheria hiyo
ina mkanganyiko kati ya
sehemu za utangulizi na vifungu
vinavyobeba maudhui husika.(Rejea
sehemu ya III kifungu cha 15 ) kwenye
utangulizi maneno yanasomeka No
broadcast on poling day na kwenye kifungu
cha maudhi cha 15 (2)kinafafanua kwamba, twelve hours immediately proceeding
polling day, they do not broadcast any politically –
related matter which may reasonably
upset the balance to be
observed throughout the election
broadcast period pursuant to
this code.
·
Sheria imeweka mitego mipana na maana
ya mambo ambayo hayatakiwi, Mfano kifungu
cha 15 (2) maneno yafuatayo.. No
broadcast any politically –
related matter which
may reasonable upset the
balance to be observed …… Hapo ni wazi kuna mkizano wa maana pana inayoweza kutafsiriwa na mamlaka moja
tu yani watunga sheria
na sio watumiaji wa sheria.
·
Sheria pia
imenyakua miongozo ya kitaaluma
kwa mwandishi na kuifanya sheria
badala kuiacha katika
maadili ya kitaaluma (Media ethics)
ambayo ingeweza kusimamiwa
na vyombo husika
kama MCT, UTPC, OJADACT, MISA, TAMWAN na vingine. Rejea msisitizo wa
sehemu ya II kifungu
cha 4(a) – (i)
RAI:
·
Kuwe
na maridhiano ya pamoja
baina ya TCRA
na wadau wa habari ili kutazama
utekelezaji wa sheria hii
ili kutominya uhuru
wa vyombo vya
habari na haki ya kupata
taaifa kwa wananchi.
·
Serikali iache
kuwa na ajenda ya
siri katika kuvibana
vyombo vya habari
wakati huu wa kuelekea
kwenye uchaguzi mkuu badala
yake ishirikiane na
vyombo hivyo kutengeneza
ajenda ya kuwavusha
watanzania salama kwenye uchaguzi
huu.
·
Wamiliki wa vyombo vya habari na waandishi wa habari wawe makini
na sheria hii
MSIMAMO WA CHAMA
Sheria hii
siyo rafiki kwa
vyombo vya habari
na inalenga kuvibana vyombo
hivyo kutofanya kazi
iapasavyo kuelekea uchaguzi
mkuu wa mwezi Oktoba, 25
mwaka huu, kama zilivyo
sheria nyingine kama ifuatavyo
sheria ya makosa
ya mtandaoni na takwimu zinazoanza
kutumika mwezi Septemba 1, mwaka huu
ina ile miswada
miwili ya haki ya kupata
taarifa na huduma
kwa vyombo vya
habari.


Edwin Soko
Chairperson

