SERENA AFUNGA MWAKA,Ajiondoa mashindano ya China Open na Fainali za WTAza Singapore
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/normal-0-false-false-false-en-us-x-none.html
Mamlaka ya mashindano
ya China yalitoa ujumbe kwa njia ya tweeter wakithibitisha, lakini Umoja wa
Tennis ya wanawake haijathibitisha taarifa ya Serena kujiondoa katika
mashindano hayo.
Inaarifiwa kuwa mchezi
namba tatu kwa ubora wa mchezo huo kwa wanawake Maria Sharapova nae ametangaza
kujitoa kutokana na majeraha ya sehemu ya mbele ya mkono wake wa kushoto.
Serena mwenye miaka 34
hajacheza mchezo wowote tangu aliposhindwa kwenye nusu fainali ya US Open kwa
muitaliano Roberta Vince moja ya matokeo ya kushitusha zaidi katika mchezo huo.
Serena alisema “si
siri, nimecheza sehemu kubwa ya mwaka huu nikiwa na maumivu… yaweza kuwa
kiwiko, fundo la mguu na sehemu kadhaa maumivu makali”
Mwalimu wa serena,
Patrick Mouratoglou alieleza mapema wiki hii kuwa, Serena amefedheheshwa sana
na matokeo ya US open yaliyopelekea kutoshinda shindano la tano mfululizo na
akatahadharisha kuwa angejitoa kwenye mashindano mengine.
Pamoja na kujitoa
mashindano mawili ya kuhitimisha mwaka huu, Serena ataumaliza mwaka huu akiwa
mchezaji namba moja kwa wanawake katika mchezo huo.
Kujitoa kwa Serena
Williams kumewahuzunisha watu wengi kwenye mchezo huo akiwemo aliyemshinda
kwenye US Open Vinci mwenye miaka 32 ambo[po alisema “Nampa pole Serena, lakini
Serena ni Serena na kwamba bado ni mchezaji bora hata asipocheza”
Souce AFP
