Ronaldo Aweka Rekodi Mpya..


Katika match ya jana Cristian Ronaldo aliandikisha magoli mawili katika mchezo huo na kufikisha idadi sawa ya magoli ya kufunga na Raul. Katika mshikemshike wa jana, Ronaldo aliifungia Real Madrid magoli hayo na kuandikisha jumla ya magoli 323 sawa na Raul aliyeichezea Madrid zaidi ya match 400 kufikisha idadi hiyo huku Ronaldo akiwa amecheza mechi chache kufikisha magoli hayo.

Pia ronaldo amefikisha zaidi ya magoli 500 katika michuano yote aliyocheza. Ronaldo aliyesajiliwa kutokea Manchster United aliyoichezea kati ya mwaka 2003 na 2009 kabla hajajiunga na miamba hiyo ya jiji la Madrid kwa uhamisho wa $90 million au Pound 59million.

Alipoulizwa kuhusu kuihama Real Madrid kuelekea timu yoyote alijibu ifuatavyo”Nina furaha hapa, nataka kushinda kila kitu hapa. Ninajisikia vizuri hapa, ila kama nilivyowahi kusema zaidi ya mara million, hakuna mtu anayejua yatayotokea siku za mbele” aliyaongea hayo alipokuwa akiongea na Cadena SER

“ Tutaona yatayotokea kesho, ila kwa sasa, nina furaha ndani Real Madrid” Aliongeza
“hakuna anayejua yatayotokea mwaka ujao. Nina furaha hapa, ila huwezi jua yatayotokea mbeleni”
“Natakiwa kufikia malengo Fulani hapa, Ninajisikia vizuri, ninataka kushinda vitu na Real Madrid kwakuwa ninadhani kilabu hii inanafasi ya kushinda mashindano, ila sijui yatayotokea”

Maelezo haya ya Ronaldo yanaiweka Real Madrid katika wakati mgumu maana anaweza kuondoka na kuelekea vilabu kadhaa ambavyo vimeonesha kumuhitaji. Ambapo amekuwa akihusishwa na kurudi Manchester United, huku PSG na Machester City wakimtolea macho pia.

Alipoulizwa kuhusu dhihaka za mchezaji wa team hasimu ya Barcelona kuhusu kukutwa kwake sehemu ya starehe baada ya kushindwa alijibu “ si muda sahihi kuongelea mambo haya. Siongelei hili kwakuwa si kitu sahihi, kwahiyo kila mtu anaweza kufikiria atakavyo”
“ilikuwa maamuzi yangu. Sikutaka kuliongelea na hakuna mtu naelazimika kujieleza kwake. Naongea napojisikia kuongea, hata team yangu haijawahi kunilazimisha kuongea.”
Alipoulizwa kwanini haongei mara nyingi na vyombo vya habari aliji, “Kwanini siongei mara kwa mara? Ni kwa sababu maswali mnayouliza sio mazuri. Sasa hili la kwenda kwenye starehe na Roldan linahusiana nini na mchezo?” “Mnataka mniweke kwenye tatizo kama Pique alivyofanya, Kwanini inihusu?”

Real Madrid imejiweka katika nafasi nzuri ya kuvuka makundi katika kombe la EUFA baada ya kushinda michezo miwili za makundi.

Mwandishi Juma…  


Related

Michezo na Burudani 5747504237401010025

Post a Comment

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress