Tanzania inaongoza kwa Wagonjwa wa Saratani ya Mlango wa kizazi Afrika Mashariki.

MANSOUR JUMANNE, MWANZA.

TAASISI ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) imesema Tanzania inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi Afrika Mashariki.

 

Imeelezwa kuwa hali hiyo inaonatokana kusababishwa na hali ya umaskini walionao Watanzania wengi, uelewa mdogo pamoja na mila potofu juu ya ugonjwa huo.

Akisoma taarifa  ya WAMA, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dk. James Kengia alisema hayo jana jijini hapa wakati akifungua mafunzo ya kuhamasisha timu za afya za Wilaya za Mikoa ya Mwanza,  kuhusu namna ya kupambana na saratani ya mlango wa kizazi.

“Takwimu za ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi kwa Tanzania zinasikitisha sana. Tunaarifiwa kwamba idadi ya wanawake 6,241 hugundulika kuwa na saratani kwa mwaka.

“Kati yao wanawake 4,355 hufariki kila mwaka katika nchi za Afrika Mashariki….Tanzania inaongoza kwa wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi,” alisema DK. Kengia.

Naye  Mkurugezi wa Uboreshaji wa Afya wa Taasisis hiyo WAMA, Dk. Sarah Maongezi alisema wagonjwa wengi wa ugonjwa huo, wanafika hospitali wamechelewa hali inayosababisha wagonjwa wengi kufariki dunia.
Kufuatia hali hiyo, aliwataka wanawake kupima mapema afya zao ili kujua iwapo wana tatizo lolote la kiafya na baadaye wawahi matibabu.

“Karibia wanawake 6,000 hufika katika Taasisi ya saratani ya Ocean Road, lakini kati ya hao wanawake 4,000, hufariki dunia baada ya miezi mitatu kutokana na kuchelewa matibabu.

“Hivyo wanawake wasisubiri hadi dalili bali pindi waonapo vituo vinavyopima basi wafike wakapime afya zao,” alisema Dk. Maongezi.

Akizungumza kwa niaba ya watoa huduma wa saratani ya mlango wa kizazi waliohudhulia mafunzo hayo, Dk. Jaliath Lange kutoka Chama Cha Madaktari Wanawake (MEWATA) alisema wametoa mafunzo kwa madaktari wa Mkoa wa Mwanza jinsi ya kupima na kutibu ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi.

“Kwa upande wa Mkoa Mwanza tunataka tuurudishe huu mpango katika ngazi ya jamii, katika vijiji na wilayani ili tujue kama tatizo limeongezeka au linapungua,” alisema Dk. Lange.

Related

Tanzania 6769311620880256422

Post a Comment

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress