Rais Kikwete kulihutubia Bunge la Kenya.
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/rais-kikwete-kulihutubia-bunge-la-kenya.html
Rais
anayemaliza muda wake wa Tanzania atakuwa mgeni wa heshima wa kwanza
kulihutubia Bunge la Kenya atapoitembelea Kenya wiki ijayo.
Spika wa
Bunge Justin Muturi amelitaarifu Bunge juu ya ratiba ya kukutana kwa seneti
siku ya jumanne ya wiki ijayo. Inatarajiwa Kikwete kuwa atatumia fursa hiyo
kuiaga Kenya kupitia Bunge hilo.
Tanzania
inatarajiwa kufanya uchaguzi mkuu wake Oktoba 25 mwaka huu. Ilitarajiwa Rais wa
Marekani Barack Obama angelikuwa rais wa Kwanza wa nje kulihutubia Bunge hilo
la 11 alipoitembelea Kenya, lakini ilishindikana dakika za mwisho kwa kile
ilichodaiwa kuwa hofu ya kiusalama.![]() |
| Rais Kikwete |
Hivi
karibuni Kikwete aliielezea kazi yake kama “kazi inayowazisha na ngumu”
akiongeza kuwa, alikuwa akiomba sana kipindi chake kiishe. “Vipindi viwili
vinatosha” Alisema akiwa Woodrow Wilson International Centre for Scholar,
Washington DC mapema mwaka huu.
Katika
Kipindi hicho pia, Rais Kikwete alieleza kuwa “Baada ya miaka 10, unahitaji
kuendelea na maisha mengine. Imekuwa miaka 10 tangu niwe katika wadhfa huu
mkubwa zaidi, Nilikuwa nina miaka 55 tu, ila nachoweza kukueleza, kazi hii
inaumiza sana akili na inachosha”
Rais
wa Tanzania yuko nchi kenya katika ziara mbalimbali za kuaga, kabla ya kufikia ukomo wa uongozi wake mapema mwaka huu mara baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25
Mwandishi: Juma Shabani
