Maafa ya Mahujaji Makka yaongezeka

Nchi ya Irani inasadikiwa ndio iliyopata maafa makubwa kwenye maafa yaliyotokea Hijja ya mwaka 2015 kutokana na kukanyagana kwa mahujaji huko Minnah. Habari za idadi ya mahujaji ilipanda ghafla jumatano hii ambapo Irani ilitangaza mahujaji wa kiirani wapatao 465 walipoteza maisha katika tukio hilo hali inayopelekea mahusiano yasiyoridhisha kati ya mahasimu hao wawili Iran na Saudi Arabia.
Wakati tawala ya Saudia ilitangaza mahujaji 769 kupoteza uhai, Mashirika ya kitangazaji yakihusiana nay a maafa ya kila nchi yalionesha wastani wa mahujaji 999 walitoweka karibu na mji mtakatifu wa Makka.

Makadiro yanaonesha kuwa maafa ni makubwa zaidi kwani uchunguzi wan chi 15 tu zilizopata maafa umetumika huku nchi zaidi ya 180 zilipeleka mahujaji wanaofikia million mbili katika hijja ya mwaka huu.

Nchi za Pakistan, India, Indonesia na Iran zote zimedai kuwa maafa yanaweza kuwa juu ya ilivyotangazwa na ufalme wa Saudia.
Mkurugenzi wa mawasiliano wa wizara ya afya bwana Faisal Alzahran, aliiambia AP Jumatano hii kuwa, ofisi yake inaidadi ya waliofariki 769 na majeruhi 934 waliojeruhiwa Minnah. Alieleza kuwa, mamlaka za kiusalama zitaendelea kutangaza kwa kadri idadi itavyoongezeka wakati zikendelea kuchunguza sababu za maafa hayo.
Katika nchi zote, Iran inaonekana ndio iliyopoteza mahujaji wengi zaidi. Kulingana na taarifa iliyotolewa na AP, idadi ya watu 600 kutoka duniani kote wamepotea baada ya tukio la Septemba 24.

Baada ya Iran, nchini zingine zilizopata maafa ya mahujaji ni pamoja na; Misri watu 124, Nigeria watu 64, Mali watu 60, Pakistan watu 52, India watu 51, Cameroon watu 42, Bangladesh watu 41, Ethiopia watu 13, Chad watu 11, Kenya watu 6, na Tanzania ikiandikisha watu 5 waliofariki.

Taarifa za leo hii kutoka Jakarta Indonesia zinaeleza kuwa Mahujaji 91 kutoka nchini humo na wengine 38 hawajulikani walipo. Kulingana na idadi kubwa ya Mahujaji kupotea, mpaka sasa inasadikiwa walioaga dunia kufikia 1036.

Haya ni maafa makubwa sana kwa miaka ya karibuni kutokea huko Makka wakati wa hija na imeinua hali ya kutoaminiana kati ya Iran na hasimu wake Serikali ya Kifalme ya Saud Arabia.

Inna Lillah, wainna ilayh rajiun. Kwa majeruhi, Mwenyezi Mungu awajaalie wapone haraka na kwa waliopotea, Mwenyezi Mungu ajaalie wapatikane wakiwa hai. (Amiin)

Mwandishi: Juma Shabani



Related

Tanzania 5483166039542995371

Post a Comment

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress