Ndege ya Marekani yatua ghafla baada ya rubani kufariki.

Ndege ya Shirika la ndege la Marekani aina ya Airbus yenye namba A320 ambayo ilikuwa na abiria 147 iliyokuwa ikitokea Phoenix kuelekea jiji la Boston ililazimika kutua kwa ghafla Syracuse baada ya rubani mmoja kati ya wawili kupata ugonjwa na hatimaye kuaga dunia safarini. Ndege hiyo ilitua salama saa 1 asubuhi.
Rubani huyo ambaye, umri, jinsi na jina lake havijawekwa wazi mpaka sasa alianza kuumwa na kupewa huduma ya kwanza na nesi ndani ya ndege akisaidiana na wahudumu wengine. Jitihada za kuokoa maisha yake zilishindwa na kupelekea kifo cha rubani huyo hali iliyopelekea rubani aliyebaki kuamua kuishusha ndege kwa dharura.


Shirika la ndege lilisema, “tukio hilo ni la kusikitisha” na sasa wanaangalia juu ya kuihudumia familia ya rubani na wafanyakazi” iliripoti ABC.

Sheria za Marekani, zinalazimisha mashirika yote ya ndege kuwa na marubani wawili kila ndege inaporuka. Msemaji wa shirika alisema “Kwa kiasi kikubwa tumejiandaa kushughulikia hali kama hizi zinapotokea.” Ndio maana kunakuwa na rubani zaidi ya mmoja kwenye ndege” alihimisha msemaji.

Habari hii imeandaliwa kwa msaa wa ABC na BBC.

Na Juma Shabani
Chanzo BBC

Related

Kimataifa 2370388145820241331

Post a Comment

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress