TANAPA watoa tamko kuhusu mamia ya Nyumbu kufa
https://alloycenyanda.blogspot.com/2015/10/tanapa-watoa-tamko-kuhusu-mamia-ya.html
TANAPA
watoa tamko kuhusu mamia ya Nyumbu kufa Mto Mara,Serengeti wasema Matukio ya
vifo vya nyumbu ni ya kawaida katika maisha ya wanyama jamii ya nyumbu
Shirika la Hifadhi la Taifa, TANAPA, limetoa ufafanuzi kuhusu habari iliyochapishwa na tovuti ya Africa Geographic Septemba 28, 2015 iliyosema mamia ya nyumbu wamekutwa wakiwa wamekufa Tanzania
Shirika la Hifadhi la Taifa, TANAPA, limetoa ufafanuzi kuhusu habari iliyochapishwa na tovuti ya Africa Geographic Septemba 28, 2015 iliyosema mamia ya nyumbu wamekutwa wakiwa wamekufa Tanzania
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya
habari na TANAPA ilisema taarifa ya wavuti hiyo iliambatanisha na picha za Mto
Mara zikionyesha mizoga ya nyumbu hao ambapo taarifa ya wavuti hiyo ilinukuliwa
ikisema Mamlaka husika (TANAPA) bado haijathibitisha idadi kamili ya vifo.
Ufafanuzi:
Kwa mujibu wa taarifa ya TANAPA,
kuhama kwa Nyumbu Serengeti ni jambo ambalo hutokea kila mwaka. Mamilioni ya
Nyumbu na Pundamlia huhama kutoka Mbuga ya Serengeti nchini Tanzania kuelekea
Maasai Mara iliyopo Kenya kutafuta maji na malisho.
Katika kuhama huko, maafa huweza
kutokea na kuzama ndani ya Mto Mara ni kati ya ajali ambazo huweza kutokea.
Inakadiriwa kuwa zaidi ya nyumbu 250,000 hufa katika kipindi hiki.
Pamoja na hayo, vizazi vipya zaidi
ya 350,000 hutokea kila mwaka hivyo kufidia idadi ya waliopotea wakati wa
kuhama kati ya mbuga hizo mbili.
Kwa kuzingatia hayo, Shirika
linautaarifu umma kuwa vifo vilivyotokea ni sehemu ya maafa ambayo huwa
yanatokea katika kipindi kama hicho kila mwaka, hakuna ambacho wangeweza
kufanya kama shirika kuzuia vifo hivyo.
Chanzo:Cloudsfm.com
Mwandishi wetu kitaifa
STANSLAUS CHACHA
