Watekelezaji wa sheria ya makosa ya mtandao wapewa mafunzo.

NA MANSOUR JUMANNE,-MWANZA.
Wizara ya Mawasiliano,Sayansi, na Teknolojia imeanza kutoa mafunzo rasmi kwa makundi mbalimbali ya watekelezaji wa sheria ya makosa ya  mtandao na sheria ya Miamala ya  kielektroniniki ili kuwajengea uwezo wa utekelezaji  wa sheria hizi katika kuzuia uhalifu wa mtandao, uchochezi, udhalilishaji, utumiaji ujasusi data, pamoja na utumaji wa picha chafu.

Akizungumza katika mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Mwanza  kwa niaba ya Kaimu Katibu Mkuu wa wizara ya mawasiliano, Prisca Ulomi ambaye ni  msemaji wa wizara hiyo, alisema makundi yaliyohudhulia mafunzo hayo ni pamoja Mahakimu,Waendesha Mashtaka, Maofisa kutoka jeshi la polisi na ofisi ya mwansheria mkuu wa serikali kutoka  mikoa ya Mwanza, Geita, Simiyu, pamoja na Mkoa wa Mara.

“Sasas hivi watu wanafanya wizi wa mitandao ,watu wanatumia mawasiliano kuiba kwenye mabenki, mtu anaweza kuwa nchi nyingine na akaiba fedha kwenye nchi nyingine kwa kutumia mitandao, lakini kuna utumiaji wa picha za ngono, udhalilishaji, uchochezi hivyo lengo letu kama wizara  ni kuhakikisha makosa haya yanakwisha kabisa kama si kupungua ,” Alisema Prisca.

Kwa upande wake  mwanasheria wa wizara hiyo, Bi Yunus Masigati, alieleza juu ya Sheria ya mtandao ya Mwaka 2015 pamoja na Sheria ya miamala ya ya kielektroniki ya  mwaka 2015 alisema sheria hizi hazikuja kwa sababu ya uchaguzi bali sheria hizi zilianza kufanyiwa kazi mwaka 2003 Chini ya sera ya TEHAMA,

“Sheria hizi hazikuja kwa ajili ya Uchaguzi kama wengi wanavyosema ,sheria hizi kwetu zina faida kiuchumi,lakini sheria hizi zinatulinda juu ya wale wahujumu miundo mbinu ya  “TEHAMA” ambayo adhabu yake wakikamatwa  ni Shilingi milioni 100, kifungo cha miaka mitano au vyote kwa pamoja,lakini sheria hizi  zinatuwezesha kulinda utu wa binadamu, pamoja na kupunguza uharifunchini Tanzania”Alisema Yunus.

Nae Mwanasheria kutoka jeshi la Polisi nchini Tanzania  Bwana Alfred Ahonga, alisema Jeshi la polisi tayari linayo mitambo ya kutosha na tayari walikwisha toa  mafunzo kwa vijana wa jeshi la polisi ili wawe wapelesi wazuri kwa ajili ya kuwabaini Waharifu wa mitandao.

Pamoja na kuahidi kutenda haki pia washiriki wa mafunzo hayo walisema wameyapokea vizuri mafunzo hayo na sheria hizi  zitawasaidia zaidi katika kuamua makosa ambayo yatakuwa yanajitokeza katika mitandao.

Related

Tanzania 3193751947531790637

Post a Comment

  1. Napendekeza bwana Nyanda ukisha itupia kwenye Blog uwe una share kwenye Mitandao mingine kwa ajili yakuiuuza Blog

    ReplyDelete

emo-but-icon

Tafuta Habari

Wasomaji

Tufuatilie Facebook

Maoni Yako

Name

Email *

Message *

item
Wordpress